TANGAZO LA AJIRA – HALMASHAURI YA WILAYA YA LUDEWA 2026

 

TANGAZO LA AJIRA – HALMASHAURI YA WILAYA YA LUDEWA 2026

UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
OFISI YA WAZIRI MKUU
TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA
HALMASHAURI YA WILAYA YA LUDEWA

Ref. No.: LDC/L.10/12 Vol. VI/30 | Tarehe: 31 Desemba 2025

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa anawatangazia Watanzania wenye sifa kuomba nafasi za kazi nane (8) katika Halmashauri hii baada ya kupata kibali kutoka Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.

1.0 DEREVA DARAJA LA II – NAFASI 4

Majukumu na Kazi

  • Kukagua gari kabla na baada ya safari ili kubaini hali ya usalama wa gari.
  • Kuwapeleka watumishi maeneo mbalimbali kwenye safari za kikazi.
  • Kufanya matengenezo madogo madogo ya gari.
  • Kukusanya na kusambaza nyaraka mbalimbali.
  • Kujaza na kutunza taarifa za safari zote katika daftari la safari (log book).
  • Kufanya usafi wa gari.
  • Kufanya kazi nyingine kadri atakavyoelekezwa na Msimamizi wake.

Sifa za Mwombaji

  • Cheti cha Kidato cha Nne (Form IV) na Leseni ya Udereva Daraja E au C.
  • Uzoefu wa kuendesha gari kwa mwaka mmoja (1) bila ajali.
  • Vyeti vya mafunzo vinavyompa sifa ya kupata daraja husika.
  • Halikadiri, awe amehudhuria Basic Driving Course kutoka VETA au chuo kinachotambuliwa na Serikali.

Ngaazi ya Mshahara: TGS B

2.0 MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II – NAFASI 4

Majukumu na Kazi

  • Kuchapa barua, taarifa na nyaraka za kawaida na za siri.
  • Kupokea wageni, kusikiliza shida zao na kuwaelekeza sehemu husika.
  • Kutunza taarifa za matukio, miadi, wageni, tarehe za vikao, safari za mkuu wake na ratiba zingine.
  • Kutafuta majalada na nyaraka zinazohitajika kwa utekelezaji wa kazi.
  • Kupokea na kusambaza majalada kwa maofisa wa idara husika.
  • Kukusanya, kutunza na kurejesha majalada sehemu husika.
  • Kuandaa dondoo na maandalizi ya vikao mbalimbali.
  • Kuandaa orodha ya mahitaji ya vifaa vya ofisi.

Sifa za Mwombaji

  • Elimu ya Kidato cha Nne au Kidato cha Sita.
  • Stashahada ya Uhifadhi / NTA Level 6 katika Uhifadhi wa Ofisi.
  • Uwezo wa Kiswahili na Kiingereza, 100 maneno kwa dakika moja kwa Hatimkato.
  • Ujuzi wa kutumia Microsoft Word, Excel, PowerPoint, Windows, Internet, E-mail na Publisher.

Ngaazi ya Mshahara: TGS C

Masharti ya Jumla

  1. Raia wa Tanzania wenye umri usiozidi miaka 45.
  2. Ambatanishe Cheti cha Kuzaliwa.
  3. Detailed CV yenye anuani, namba za simu na majina ya wadhamini.
  4. Vyeti vya taaluma na Kidato cha Nne/Sita pamoja na mafunzo husika, vipandikwe kwenye Ajira Portal.
  5. Testimonials, Provision Results, Statement of Results HAVIKUBALIKI.
  6. Waombaji kazi wa Dereva II lazima waambatanishe vyeti vya mafunzo ya Udereva.
  7. Picha mbili (2) za Passport Size za hivi karibuni.
  8. Vyeti vya waliosoma nje ya nchi vinapaswa kuthibitishwa na TCU, NECTA, NACTE.
  9. Waombaji waliostaafishwa katika Utumishi wa Umma hawaruhusiwi kuomba bila kibali cha Katibu Mkuu Kiongozi.
  10. Waajiriwa walioko katika nafasi za kuingilia hawaruhusiwi kuomba.
  11. Uwasilishwaji wa taarifa au nyaraka za kughushi utachukuliwa hatua za kisheria.
  12. Mwisho wa kutuma maombi: 11 Januari 2026.

Maelekezo Muhimu

Kumbuka kuambatanisha barua ya maombi iliyosainiwa pamoja na vyeti vya elimu. Barua ielekezwe kwa:

Mkurugenzi Mtendaji,
Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa,
S.L.P 19,
LUDEWA.

Muundo wa Maombi

Maombi yote yatumwe kwa njia ya kielektroniki kupitia Ajira Portal:

https://portal.ajira.go.tz/

Maombi yasiyoendana na utaratibu huu hayatafanyiwa kazi.

Limetolewa na:
MKURUGENZI MTENDAJI (W)
HALMASHAURI YA WILAYA YA LUDEWA

Previous Post Next Post

نموذج الاتصال