TAMISEMI Yatangaza Nafasi 1,500 za Walimu wa Kujitolea Sekondari 2026 | GPE - TSP

TAMISEMI Yatangaza Nafasi 1,500 za Walimu wa Kujitolea Sekondari 2026 | GPE - TSP

TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA SEKONDARI 2026

Kupitia Mradi wa GPE – TSP | OWM – TAMISEMI

Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM – TAMISEMI), kupitia Mradi wa Kuboresha Kada ya Ualimu Global Partnership for Education – Teacher Support Programme (GPE – TSP), inatekeleza afua mbalimbali ikiwemo kuratibu upatikanaji wa Walimu wa Kujitolea katika shule za sekondari zenye uhitaji mkubwa wa walimu.

Kupitia mradi huu, OWM – TAMISEMI inatangaza nafasi 1,500 za Walimu wa Kujitolea kwa shule za sekondari zilizo chini ya Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa kuzingatia Secondary Teacher Allocation Protocol (S – TAP).

Masomo Yanayohitajika

  • Sayansi na Teknolojia (STEM)
  • Masomo ya Amali (Vocational Subjects)
  • Masomo ya Biashara (Business Studies)

Majukumu ya Jumla ya Mwalimu wa Kujitolea

  • Kuandaa maandalio ya masomo, mipango ya kazi na nyaraka za kitaaluma
  • Kutengeneza na kutumia zana za kufundishia na kujifunzia
  • Kufundisha, kufanya tathmini na kutunza kumbukumbu za maendeleo ya wanafunzi
  • Kusimamia mahudhurio ya wanafunzi shuleni na darasani
  • Kutoa ushauri nasaha na kusimamia malezi ya wanafunzi
  • Kusimamia vifaa na mali za shule
  • Kufanya kazi nyingine atakazopangiwa na Mkuu wa Shule

Sifa za Waombaji kwa Masomo

Fizikia (Physics) – Nafasi 504

  • Shahada ya Elimu/Ualimu yenye Fizikia; au
  • Shahada isiyo ya Ualimu yenye Fizikia pamoja na PGDE; au
  • Stashahada ya Ualimu yenye Fizikia

Kemia (Chemistry) – Nafasi 246

  • Shahada ya Elimu/Ualimu yenye Kemia; au
  • Shahada isiyo ya Ualimu yenye Kemia pamoja na PGDE; au
  • Stashahada ya Ualimu yenye Kemia

Biolojia (Biology) – Nafasi 332

  • Shahada ya Elimu/Ualimu yenye Biolojia; au
  • Shahada isiyo ya Ualimu yenye Biolojia pamoja na PGDE; au
  • Stashahada ya Ualimu yenye Biolojia

Hisabati (Mathematics) – Nafasi 418

  • Shahada ya Elimu/Ualimu yenye Hisabati; au
  • Shahada isiyo ya Ualimu yenye Hisabati pamoja na PGDE; au
  • Stashahada ya Ualimu yenye Hisabati

Masharti ya Jumla ya Waombaji

  • Awe raia wa Tanzania mwenye NIDA na umri usiozidi miaka 43
  • Aambatishe vyeti vya elimu, taaluma na cheti cha kuzaliwa
  • Awe tayari kufanya kazi katika shule zenye uhitaji mkubwa wa walimu
  • Asiwe mwajiriwa wa Serikali au taasisi nyingine
  • Waombaji waliosoma nje ya nchi wawe na Equivalent Number (EQ) kutoka NECTA

Jinsi ya Kutuma Maombi

Waombaji wote wenye sifa watembelee tovuti ya OWM – TAMISEMI: www.tamisemi.go.tz kuanzia tarehe 01 hadi 14 Januari, 2026.

Pakua Tangazo Rasmi (PDF)

Bofya kitufe hapa chini kupakua tangazo kamili la TAMISEMI

DOWNLOAD PDF

Mwisho wa kupokea maombi: 14 Januari, 2026 saa 05:59 usiku

Previous Post Next Post

نموذج الاتصال