UPDATED | TAMISEMI Yatangaza Nafasi 1,500 za Walimu wa Kujitolea Sekondari 2026 | GPE - TSP

TAMISEMI Yatangaza Nafasi 1,500 za Walimu wa Kujitolea Sekondari 2026 | GPE–TSP
TAMISEMI Volunteer Teachers 2026
UPDATED 2026

TANGAZO LA NAFASI 1,500 ZA WALIMU WA KUJITOLEA SEKONDARI – 2026

Kupitia Mradi wa GPE–TSP | OWM–TAMISEMI

Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI), kupitia Mradi wa Global Partnership for Education – Teacher Support Programme (GPE–TSP), inatangaza nafasi 1,500 za Walimu wa Kujitolea kwa shule za sekondari zenye uhitaji mkubwa wa walimu kwa kuzingatia Secondary Teacher Allocation Protocol (S–TAP).

Masomo Yanayohitajika:
  • Sayansi na Teknolojia (STEM)
  • Masomo ya Amali (Vocational Subjects)
  • Masomo ya Biashara (Business Studies)

Idadi ya Nafasi kwa Kila Somo

  • Fizikia (Physics) – Nafasi 504
  • Kemia (Chemistry) – Nafasi 246
  • Biolojia (Biology) – Nafasi 332
  • Hisabati (Mathematics) – Nafasi 418

Majukumu ya Mwalimu wa Kujitolea

  • Kuandaa maandalio ya masomo na mipango ya kazi
  • Kufundisha na kufanya tathmini za wanafunzi
  • Kutunza kumbukumbu za maendeleo ya wanafunzi
  • Kusimamia mahudhurio na malezi ya wanafunzi
  • Kusimamia vifaa na mali za shule
  • Kutekeleza majukumu mengine atakayopangiwa na Mkuu wa Shule

Masharti ya Jumla

  • Awe raia wa Tanzania mwenye NIDA na umri ≤ miaka 43
  • Asiwe mwajiriwa wa Serikali au taasisi nyingine
  • Awe tayari kufanya kazi shule zenye uhitaji mkubwa
  • Awe na vyeti halali vya elimu na taaluma
  • Waliosoma nje ya nchi wawe na Equivalent Number (EQ) kutoka NECTA

Jinsi ya Kutuma Maombi

Maombi yote yafanywe mtandaoni kupitia Mfumo wa Ajira TAMISEMI:

APPLY NOW – TAMISEMI

📅 Tarehe za Maombi: 14 Januari 2026 hadi 28 Januari 2026

Pakua Tangazo Rasmi (PDF)

DOWNLOAD PDF
Mwisho wa Kupokea Maombi: 28 Januari 2026 saa 05:59 usiku

Post a Comment

Tafadhali Tuambie kupitia hapa

Previous Post Next Post

Featured Post

Smart Education Tanzania