UPDATED 2026
TANGAZO LA NAFASI 1,500 ZA WALIMU WA KUJITOLEA SEKONDARI – 2026
Kupitia Mradi wa GPE–TSP | OWM–TAMISEMI
Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI), kupitia Mradi wa Global Partnership for Education – Teacher Support Programme (GPE–TSP), inatangaza nafasi 1,500 za Walimu wa Kujitolea kwa shule za sekondari zenye uhitaji mkubwa wa walimu kwa kuzingatia Secondary Teacher Allocation Protocol (S–TAP).
Masomo Yanayohitajika:
- Sayansi na Teknolojia (STEM)
- Masomo ya Amali (Vocational Subjects)
- Masomo ya Biashara (Business Studies)
Idadi ya Nafasi kwa Kila Somo
- Fizikia (Physics) – Nafasi 504
- Kemia (Chemistry) – Nafasi 246
- Biolojia (Biology) – Nafasi 332
- Hisabati (Mathematics) – Nafasi 418
Majukumu ya Mwalimu wa Kujitolea
- Kuandaa maandalio ya masomo na mipango ya kazi
- Kufundisha na kufanya tathmini za wanafunzi
- Kutunza kumbukumbu za maendeleo ya wanafunzi
- Kusimamia mahudhurio na malezi ya wanafunzi
- Kusimamia vifaa na mali za shule
- Kutekeleza majukumu mengine atakayopangiwa na Mkuu wa Shule
Masharti ya Jumla
- Awe raia wa Tanzania mwenye NIDA na umri ≤ miaka 43
- Asiwe mwajiriwa wa Serikali au taasisi nyingine
- Awe tayari kufanya kazi shule zenye uhitaji mkubwa
- Awe na vyeti halali vya elimu na taaluma
- Waliosoma nje ya nchi wawe na Equivalent Number (EQ) kutoka NECTA
Jinsi ya Kutuma Maombi
Maombi yote yafanywe mtandaoni kupitia Mfumo wa Ajira TAMISEMI:
APPLY NOW – TAMISEMI📅 Tarehe za Maombi: 14 Januari 2026 hadi 28 Januari 2026
Pakua Tangazo Rasmi (PDF)
DOWNLOAD PDF
Mwisho wa Kupokea Maombi:
28 Januari 2026 saa 05:59 usiku
Post a Comment
Tafadhali Tuambie kupitia hapa