banner

Mbinu za Kutoa Maelekezo Bayana Darasani | Mawasiliano ya Kitaaluma

 

SOMO: MAWASILIANO YA KITAALAMU

UMAHIRI MKUU: Kumudu kuwasiliana kitaalamu UMAHIRI MAHUSUSI: Kuwasilisha taarifa za kitaaluma darasani kwa kutumia lugha stahiki SHUGHULI YA UJIFUNZAJI: Kumudu mbinu za kutoa maelekezo bayana darasani wakati wa ufundishaji na ujifunzaji

MBINU ZA UWASILISHAJI WA TAARIFA ZA KITAALUMA

a) Kutumia Zana-Uoni:

  • Zana hizi ni kama chati, grafu, video, modeli halisi, ubao mweupe au mweusi

  • Husaidia kuhusisha maudhui na maisha halisi ya wanafunzi

b) Kupangilia Uwasilishaji wa Maudhui:

  • Anza kwa utangulizi shirikishi

  • Fuata kiini kilichopangiliwa vizuri

  • Hitimisha kwa muhtasari wenye hoja kuu na mwito wa kuchukua hatua

c) Kutumia Mbinu Shirikishi:

  • Majadiliano

  • Vitendo

  • Nyimbo

  • Hadithi

  • Maswali na majibu

  • Kazi za vikundi

  • Ufundishaji kiduchu

  • Matumizi ya zana

d) Shughuli za Vitendo:

  • Huwashirikisha wanafunzi moja kwa moja katika mchakato wa ujifunzaji

e) Kutumia Teknolojia:

  • Programu za kompyuta za kielimu

  • Michezo yenye mafunzo

  • Hukuza uelewa wa dhana mbalimbali

f) Kutoa Mrejesho Chanya:

  • Huchochea ukuaji wa kitaaluma na maendeleo binafsi

  • Husaidia wanafunzi kutambua uwezo na udhaifu wao

  • Hujenga imani, uhusiano mzuri na mazingira wezeshi ya ujifunzaji

DHANA YA MAELEKEZO BAYANA

  • Ni mbinu ya kufundisha inayomhusisha mwalimu kuelekeza kwa uwazi na hatua kwa hatua jinsi ya kufanya jambo fulani darasani

  • Lengo ni kuhakikisha wanafunzi wanaelewa wazi wanachopaswa kufanya, jinsi ya kufanya, na kwa nini wanapaswa kufanya hivyo

MBINU ZA KUTOA MAELEKEZO BAYANA KATIKA HATUA TATU KUU

A) Wakati wa Ufundishaji:

  • Tumia lugha rahisi na inayoeleweka

  • Eleza malengo ya somo kabla ya kuanza

  • Onyesha mfano wa kile kinachotarajiwa

  • Tumia vifaa vya kufundishia kusaidia maelekezo

  • Tumia mbinu shirikishi

B) Wakati wa Ujifunzaji:

  • Toa kazi ndogo ndogo kwa hatua

  • Hakikisha wanafunzi wanaelewa kila hatua

  • Tembea darasani kutoa msaada

  • Waruhusu wanafunzi kuuliza maswali

  • Toa mrejesho wa haraka

C) Wakati wa Upimaji:

  • Elekeza kwa uwazi aina ya mtihani au jaribio

  • Toa maelekezo ya maandishi na ya mdomo

  • Hakikisha maelekezo ya maswali ni wazi

  • Toa muda wa kutosha kwa kila sehemu

  • Wape wanafunzi nafasi ya kuuliza kabla ya kuanza

UMUHIMU WA MAELEKEZO BAYANA

  • Husaidia wanafunzi kuelewa matarajio ya kazi na somo

  • Huboresha ufanisi wa ujifunzaji kwa kupunguza mkanganyiko

  • Huongeza ushiriki wa wanafunzi

  • Humwezesha mwalimu kufanya tathmini kwa usahihi

MIFANO YA MBINU ZA KUTOA MAELEKEZO DARASANI

  • Tumia lugha sahihi na nyepesi

  • Toa maelekezo hatua kwa hatua

  • Eleza kwa vitendo kabla ya wanafunzi kufanya wenyewe

  • Tumia mbinu ya kupima uelewa (maswali ya kufuatilia)

  • Tumia zana-uoni kama michoro na chati

  • Tumia kauli ya kutenda (mfano: “Fanya jaribio…” badala ya “Jaribio linapaswa kufanywa…”)

  • Wahimize wanafunzi kuuliza maswali

MASWALI YA MJADALA

  1. Fikiria kwamba umeteuliwa kuiwakilisha shule yako katika shindano la ufundishaji. Andaa mwongozo wa mbinu utakazotumia kutoa maelekezo kwa usahihi darasani.

  2. Eleza namna utakavyotumia mbinu za kutoa maelekezo katika kuwapima wanafunzi wako.

  3. Ni kwa namna gani utaweza kuyafanya maelekezo changamani kueleweka kwa urahisi kwa wanafunzi wako?

  4. Jadili ni kwa namna gani utaweza kuwahamasisha wanafunzi kuuliza maswali ikiwa hawajaelewa maelekezo.

  5. Fafanua namna ugumu wa maelekezo unavyoweza kuathiri motisha na ujasiri wa wanafunzi katika kukamilisha kazi.

  6. Eleza namna teknolojia inavyoweza kusaidia kuweka uwazi na ufikikaji wa maelekezo.

Previous Post Next Post
banner
×

Contact Us