SOMO: MAWASILIANO YA KITAALAMU
MASWALI YA MWONGOZO
Eleza kwa kina dhana ya taarifa za kitaaluma na umuhimu wake kwa mwalimu. (Kundi la 1 & 8)
Taja na kufafanua vyanzo vitano vya taarifa za kitaaluma. (Kundi 2 & 7)
Taja na eleza sifa tano za taarifa za kitaaluma na kwa nini ni muhimu kuzingatia sifa hizo. (Kundi 3 & 6)
Kwa kutumia mifano, fafanua jinsi taarifa za kitaaluma zinavyotumika katika mazingira ya ualimu. (Kundi 4 & 5)
Jadili changamoto tano zinazoweza kuwapata wanafunzi katika kupata au kuwasilisha taarifa za kitaaluma. (Makundi yote)
DHANA YA TAARIFA ZA KITAALUMA
Taarifa za kitaaluma ni vyanzo vya maarifa vinavyoandaliwa, kusambazwa na kutumika katika muktadha wa elimu.
Huandaliwa na wataalamu, wanazuoni na watafiti kwa ajili ya matumizi ya kielimu.
Husaidia kukuza maarifa, fikra tunduizi na kuchangia katika maendeleo ya taaluma husika.
Hupatikana katika:
Vitabu vya kitaaluma
Maandishi ya tafiti
Makala za majarida ya kielimu
Tasnifu na disertation
Mihadhara ya vyuoni
VYANZO VYA TAARIFA ZA KITAALUMA
A. Vyanzo vya Msingi:
Tafiti za awali
Majarida ya kisayansi
Mihadhara ya kitaaluma
B. Vyanzo vya Sekondari:
Vitabu vya kiada na rejea
Ripoti za kitaasisi
Makala za magazeti na majarida
Mfano wa vyanzo:
Vitabu vya kiada/ziada
Makala za tafiti
Ripoti rasmi
Ensaiklopidia
Kamusi
SIFA ZA TAARIFA ZA KITAALUMA
Uhakika na uthibitisho: Zinatokana na utafiti wa kina na ushahidi wa kisayansi
Marejeo ya vyanzo: Hutumia mifumo rasmi ya kunukuu kama APA
Lugha rasmi ya kitaaluma: Hutumia maneno sahihi yasiyo ya kihisia
Uchambuzi wa kina: Huchambua hoja kwa kutumia nadharia na ushahidi
Muktadha wa kielimu: Hutolewa katika mazingira rasmi ya elimu
MASWALI YA MJADALA
Kwa kutumia vyanzo vya kuaminika vya taarifa za kitaaluma, andika insha kuhusu namna uhusiano unavyoathiri maendeleo.
Kwa kutumia ensaiklopidia ya mtandaoni, andika historia fupi ya Mwalimu Julius Nyerere.
Kumbuka wakati ulipopewa jukumu la kuwasilisha mada fulani. Eleza namna ulivyokusanya taarifa kwa ajili ya uwasilisho huo.
Umepewa kazi mradi kuhusu ujanishaji wa mazingira. Eleza namna vyanzo mbalimbali vya kuaminika vitakavyokusaidia kutekeleza kazi hiyo.
SIFA ZA VYANZO VYA KUAMINIKA VYA TAARIFA ZA KITAALUMA
Kuaminika:
Sifa za mwandishi
Hadhi ya mchapishaji
Ushahidi wa mamlaka
Usahihi:
Ukweli wa maudhui
Umakini wa uwasilishaji
Data zisizo na makosa
Kutopendelea:
Maudhui yasiyoegemea upande wowote
Uchambuzi wa kitaalamu
Hitimisho linalotokana na data
Uwazi na Ufasaha:
Lugha stahiki kwa hadhira lengwa
Uwasilishaji wa hoja kwa uwazi
Taarifa sahihi na elekezi
Marejeleo:
Kunukuu kwa kufuata taratibu rasmi
Mpangilio mzuri:
Muundo wa kimantiki
Vichwa vikuu na vidogo
Sehemu ndogo ndogo zenye mtiririko
Kusudi na Mawanda:
Malengo ya kazi
Mawanda ya mada
Muktadha wa utafiti

