TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA WALIMU 2026
Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma kwa niaba ya MDAs & LGAs anapenda kuwataarifu waombaji wote wa Ajira za Walimu kuwa usaili unatarajiwa kuendeshwa kuanzia tarehe 14/02/2026. Waombaji watakaofaulu usaili huo watapangiwa vituo vya kazi.
MAELEKEZO MUHIMU KWA WALIOITWA KWENYE USAILI
- Usaili utafanyika kwa tarehe, muda na eneo lililoainishwa kwa kila kada.
- Kila msailiwa afike akiwa amevaa Barakoa (Mask).
- Msailiwa awe na kitambulisho halali kwa ajili ya utambuzi.
- Msailiwa afike na vyeti vyote HALISI kuanzia Cheti cha Kuzaliwa hadi Shahada kulingana na sifa.
- Result slips, provisional results au testimonials HAZITAKUBALIWA.
- Kwa waliosoma nje ya Tanzania, vyeti vihakikiwe na TCU, NACTVET au NECTA.
- Kila msailiwa atajigharamia chakula, usafiri na malazi.
- Wasioona majina yao waingie kwenye akaunti zao za Ajira Portal kuona sababu.
PAKUA TANGAZO KAMILI (PDF)
Bonyeza kitufe hapa chini kupakua orodha kamili ya Majina ya Walioitwa Kwenye Usaili wa Walimu 2026.
Endelea kufuatilia taarifa sahihi za ajira na elimu kupitia SmartEducation – www.smarteducation.co.tz

Post a Comment
Tafadhali Tuambie kupitia hapa