FAHAMU Makosa yanayosababisha Ufaulu Mbovu kwa Darasa la Nne NECTA
Matokeo ya NECTA Darasa la Nne yamekuwa yakionyesha changamoto ya kushuka kwa ufaulu katika baadhi ya shule. Uchambuzi wa kitaaluma unaonyesha kuwa chanzo kikubwa si wanafunzi pekee, bali ni makosa ya kitaalamu yanayofanywa wakati wa maandalizi.
1. Kutotumia Mtaala Ulioboreshwa (Competence-Based Curriculum)
Walimu wengi bado wanategemea mbinu za zamani zisizolenga umahiri wa mwanafunzi. NECTA inapima zaidi uwezo wa mwanafunzi kutumia maarifa, si kukariri.
2. Kupuuzia Tathmini Endelevu (Continuous Assessment)
Kutegemea mitihani ya mwisho pekee huwafanya wanafunzi kushindwa kubaini mapungufu yao mapema.
3. Kutotumia Maswali ya Mtindo wa NECTA
Wanafunzi wengi hupoteza alama kwa kushindwa kuelewa mtindo wa maswali ya NECTA.
4. Usimamizi Duni wa Muda Darasani
Mada kuchelewa kukamilika husababisha kukosa muda wa marudio kabla ya mtihani.
5. Kutowajengea Wanafunzi Ujuzi wa Kujibu kwa Maandishi
Majibu yasiyo na mpangilio na makosa ya lugha husababisha kupoteza alama nyingi.
PAKUA PDF YA MWONGOZO KWA WALIMU
Pata rasilimali kamili zenye Notes, Lesson Plans, Schemes, Mitihani + Majibu zilizoandaliwa kulingana na Mtaala Ulioboreshwa.
PAKUA PDF SASA
Post a Comment
Tafadhali Tuambie kupitia hapa