Call for Oral Interview at Mahakama December 2025 | JSC Tanzania

Call for Oral Interview at Mahakama December 2025

Judicial Service Commission (JSC) inawaarifu waombaji wote wa ajira mbalimbali kuwa, baada ya kukamilika kwa usaili wa hatua ya kwanza (First Stage Interviews) uliofanyika kuanzia tarehe 16 Desemba hadi 23 Desemba, 2025 katika vituo mbalimbali nchini, majina ya waombaji waliofanikiwa kuchaguliwa kuendelea na hatua ya pili ya usaili (Oral Interview) yametangazwa rasmi.

Hatua ya Pili: Oral Interview

Waombaji ambao majina yao yanaonekana kwenye tangazo hili wamechaguliwa kushiriki usaili wa mdomo (Oral Interview). Tarehe pamoja na vituo vya usaili vimeainishwa kwenye orodha ya waombaji walioteuliwa (Shortlisted Candidates List).

Tahadhari Muhimu kwa Kada Maalum

Waombaji wa nafasi zifuatazo:

  • Office Assistant II (Mwandishi Mwendesha Ofisi II)
  • Driver II

Watatakiwa kwanza kufanya Practical Interview. Ni waombaji watakaofaulu usaili wa vitendo pekee ndio watakaoruhusiwa kuendelea na usaili wa mdomo (Oral Interview).

Ratiba ya Usaili

  • Tarehe za Usaili: 5 Januari hadi 16 Januari, 2026
  • Muda wa Kuripoti: Saa 2:00 asubuhi (8:00 A.M.)

Nyaraka Muhimu za Kuja Nazo

Waombaji wote waliochaguliwa wanatakiwa kufika wakiwa na nakala halisi (Original Copies) za nyaraka zifuatazo:

  • Vyeti vya Taaluma (Academic Certificates)
  • Vyeti vya Kitaaluma (Professional Certificates)
  • Cheti cha Kuzaliwa
  • Kitambulisho kimoja halali cha Serikali chenye picha, kama:
  • Kitambulisho cha Taifa (NIDA)
  • Kitambulisho cha Mpiga Kura
  • Pasipoti
  • Leseni ya Udereva

Masharti Muhimu

  • Waombaji watakaoshindwa kuwasilisha nyaraka zote hawatafanyiwa usaili
  • Waombaji watakaofika nje ya muda uliopangwa hawataruhusiwa kufanya usaili
  • Kila mwombaji anatakiwa kuhudhuria usaili katika kituo alichopangiwa pekee

Waombaji ambao majina yao hayapo kwenye orodha ya walioteuliwa wanapaswa kufahamu kuwa hawakufanikiwa kuendelea na hatua ya pili ya usaili.

Download PDF ya Majina ya Waliochaguliwa

Bofya kitufe hapa chini kupakua PDF yenye orodha ya waombaji waliochaguliwa kushiriki usaili wa Oral Interview Mahakama:

Download PDF

Taarifa Zaidi

Kwa taarifa kamili na matamko rasmi, tembelea tovuti ya Judicial Service Commission:

www.jsc.go.tz

Mawasiliano

Kwa maswali au ufafanuzi zaidi, wasiliana nasi masaa 24 kupitia:

Simu: 0734 219 821 / 0738 247 341
Barua pepe: maulizo.ajira@jsc.go.tz


AjiraPort | Smart Education
Chanzo chako cha taarifa sahihi na za haraka kuhusu Ajira, Usaili na Fursa za Kazi Tanzania.

Previous Post Next Post

نموذج الاتصال