VETA Second Selection 2026 Officially Announced
Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) inapenda kuutangazia umma kuwa uchaguzi wa waombaji walioomba kujiunga na elimu na mafunzo ya ufundi stadi katika vyuo vya VETA kwa muhula ulioanza Januari, 2026 (Awamu ya Pili – Second Selection) umekamilika rasmi.
Orodha ya majina ya waliochaguliwa pamoja na maelekezo ya kujiunga (Joining Instructions) kwa kila chuo vinapatikana kupitia:
- Tovuti rasmi ya VETA: www.veta.go.tz
- Katika vyuo vya VETA kote nchini
📅 Tarehe ya Mwisho ya Kuripoti: 24 Februari, 2026
📚 Masomo Yataanza: 25 Februari, 2026
Waombaji wote waliochaguliwa wanatakiwa kufika katika vyuo walivyopangiwa ndani ya muda uliopangwa ili kukamilisha taratibu za usajili.
📌 Endelea kufuatilia Smart Education Blog kwa taarifa zote muhimu za elimu, selections, ajira na matokeo nchini Tanzania.

Post a Comment
Tafadhali Tuambie kupitia hapa