📌 TANGAZO LA KUITWA USAILI – AJIRA SERIKALINI 2025/2026
Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma kwa niaba ya Tume ya Madini (TMC), RUWASA, MNH, MLHHSD na NAOT anawatangazia waombaji kazi waliotuma maombi kwamba USAILI unatarajiwa kuendeshwa kuanzia 29/09/2025 hadi 30/01/2026.
Waombaji watakaofaulu usaili watapangiwa vituo vya kazi.
📌 MAELEKEZO YA WAOMBAJI USAILI
- Usaili utafanyika kulingana na tarehe, muda na mahali kama ilivyo kwenye tangazo.
- Kila msailiwa anatakiwa kufika akiwa amevaa Barakoa (Mask).
- Kila msailiwa anapaswa kuwa na kitambulisho (mkazi, mpiga kura, kazi, uraia, pasipoti, leseni ya udereva au barua ya utambulisho kutoka Serikali ya Mtaa/Kijiji).
- Kila msailiwa anapaswa kuleta vyeti halisi (Cheti cha kuzaliwa, kidato IV, VI, Astashahada, Stashahada, Shahada nk).
- Testimonials, Provisional Results, Statement of results hazitakubaliwa.
- Kada zinazohitaji usajili wa Bodi za Kitaaluma zinatakiwa kuleta vyeti halisi vya usajili na leseni ya kazi.
- Msailiwa atajigharamia chakula, usafiri na malazi.
- Wasailiwa waliosoma nje ya Tanzania wahakikishe vyeti vimeidhinishwa na mamlaka husika (TCU/NACTVET/NECTA).
- Wasailiwa ambao hawajaona majina yao wanapaswa kuangalia sababu kwenye Ajira Portal.
- Waliotajwa wahakikishe wanakili namba ya usaili kwenye akaunti yao.
- Majina yanayotofautiana yanatakiwa kuleta Deed Poll iliyosajiliwa na Wizara ya Ardhi.
📌 RATIBA YA USAILI (MCHUJO)
| MWAJIRI | KADA | TAREHE | MAHALI |
|---|---|---|---|
| MLHHSD | AFISA ARDHI MSAIDIZI II | 2025-09-29 07:00 | USAILI WA MTANDAO (ONLINE) Utajulishwa kituo kupitia Ajira Portal |
| MNH | ACCOUNTANT II | 2026-01-24 07:00 | USAILI WA MTANDAO (ONLINE) Utajulishwa kituo kupitia Ajira Portal |
| NAOT | MKAGUZI DARAJA LA II | 2026-01-25 07:00 | USAILI WA MTANDAO (ONLINE) Utajulishwa kituo kupitia Ajira Portal |
| RUWASA | WATER ENGINEER II | 2026-01-25 07:00 | USAILI WA MTANDAO (ONLINE) Utajulishwa kituo kupitia Ajira Portal |
| TMC | ENGINEER II (MINING ENGINEERING) | 2026-01-25 07:00 | USAILI WA MTANDAO (ONLINE) Utajulishwa kituo kupitia Ajira Portal |
📌 RATIBA YA USAILI (MAHOJIANO)
| MWAJIRI | KADA | TAREHE | MAHALI |
|---|---|---|---|
| MLHHSD | AFISA ARDHI MSAIDIZI II | 2025-10-10 07:00 | OFISI YA SEKRETARIETI YA AJIRA (PSRS) - DODOMA |
| NAOT | MKAGUZI DARAJA LA II | 2026-01-27 07:00 | OFISI YA SEKRETARIETI YA AJIRA (PSRS) - DODOMA |
| RUWASA | WATER ENGINEER II | 2026-01-29 07:00 | OFISI YA SEKRETARIETI YA AJIRA (PSRS) - DODOMA |
| MNH | ACCOUNTANT II | 2026-01-30 07:00 | OFISI YA SEKRETARIETI YA AJIRA (PSRS) - DODOMA |
| TMC | ENGINEER II (MINING ENGINEERING) | 2026-01-30 07:00 | OFISI YA SEKRETARIETI YA AJIRA (PSRS) - DODOMA |
👉 Kwa maelezo zaidi na kuangalia majina ya waliotajwa, ingia kwenye:
- Ajira Portal: www.ajira.go.tz
- Au Tovuti ya Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
📌 Kumbuka: Usaili unatarajiwa kuanza na kuisha kwa tarehe zilizotangazwa. Usikose fursa!

Post a Comment
Tafadhali Tuambie kupitia hapa